Karibu Nyumbani

KSh 400

Kuwatunza Waumini Waliotoka Kwenye Uislamu

 

Description

Karibu Nyumbani, Kuwatunza Waumini Waliotoka Kwenye Uislamu

Horst B Pietzsch, Kur 130

Waislamu wanapomgeukia Kristo, furaha yao mpya mara nyingi huwa na wasi wasi mkubwa. Mara nyingi wanakumbwa na kukataliwa na jamii zao, jamaa zao za karibu huwapuuza na hata huanza kuwapinga kwa dhati. Bila marafiki Wakristo ambao watasimama na kutembea nao katika njia hii mpya ya imani, watawezaje kujifunza kumudu msukumo huu na kuchukua msimamo dhidi ya upinzani na unyayasaji ambao huwaletea uoga na majaribu?

Na watawezaje kukua ili waweze kuwashirikisha jamaa na marafiki zao na kuweza kuwafikia umma wa kiislamu na kuhimiza wale wanaotafuta wokovu katika Kristo?

Kitabu hiki:

  • Ni kielelezo muhimu kwa Mkristo ili kumsaidia awe na maono ya kuwatunza na kuwafuatilia waumini wanaotoka katika Uislamu.
  • Kinapendekezwa kwa kila mchungaji, viongozi wa huduma na mwinjilisti anayetaka kuona waumiini waliotoka kwenye Uislamu wakisimama Imara katika imani yao.
  • Ni chombo muhimu kinachoonyesha njia mwafaka jinsi ya kuwajumuisha waumini waliotoka kwenye Uislamu katika kanisa na kuwakuza vema kiroho.